Thursday, November 10, 2011

Mkutano wa 05/11/2011:Kutoa mrejesho wa utendaji mwaka 1 na kukusanya maoni ya wananchi!






Huu ni mkutano ambao niliufanya katika kata ya Ubungo ndani ya Jimbo la UBUNGO baada ya maombi ya wananchi wengi kuufanyia mkutano huo katika kata hiyo.

Licha ya kufuata taratibu zote za kutoa taarifa polisi, Jeshi la Polisi lilitoa amri ndani ya muda mfupi sana kusitisha mkutano huu. Sikurudi nyuma! Niliufanya mkutano huu. Nashukuru sana wananchi ambao walijitokeza kwa wingi sana. Nawashukuru sana wananchi ambao licha ya hofu na vitisho ambavyo Jeshi la Polisi ilivitoa walikuwa mstari wa mbele kuhudhuria mkutano. Nawashukuru pia wananchi walionipa kipaza sauti baada ya vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya mkutano kukamatwa na Jeshi la Polisi.

Napenda kuwapa pole viongozi wenzangu wote sambamba, wanachadema na wananchi wote ambao walipata misukosuko ya kukamatwa na Polisi siku ile, Novemba 5, 2011. Daima; Aluta continua!

Tukumbuke: "SIASA SI UADUI"!

No comments: