Saturday, March 24, 2012

Ratiba ya Mbunge kukutana na wananchi leo Kwembe na Saranga/Kimara

Ratiba yangu ya kukutana na wananchi jimboni Ubungo leo jumapili tarehe 25 Machi 2011: Saa 9 mpaka 10 nitakuwa Kata ya Kwembe Mtaa wa Luguruni Msakuzi kwa Mbokomu kuhusu Umeme na Maji kupitia mkutano wa kuunganisha nguvu za pamoja na wananchi kuwezesha hatua kuchukuliwa na DAWASCO na TANESCO.


Mkutano wa Hadhara Kimara mwisho Saa 9:00 mpaka 12 Jioni kutoa mrejesho kuhusu maji, barabara na kesi ya kupinga ushindi wetu. Mkutano utaanza na hotuba za viongozi wa chama jimbo la madiwani wa kata za Saranga na Kimara, mimi nitaanza kuhutubia kuanzia saa 11 jioni na kutakuwa na fursa ya kuniuliza maswali ya papo kwa papo na kuwasilisha masuala mbalimbali ya kuzingatiwa na mbunge na chama katika mkutano wa saba wa bunge. Nimeitika mwito, natarajia uwepo wenu. Maslahi ya Umma Kwanza.

No comments: