Friday, May 25, 2012

Shamrashamra za Ushindi wa Kesi ya Mnyika jana

Shangwe!!Mnyika akinyanyuliwa juu baada ya Jaji kumtangaza ni Mbunge halali wa Ubungo tena.

Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika akiwa amebebwa juu juu na wanachama wa CHADEMA  pamoja na washabiki wake nje ya mahakama kuu Kanda ya Dar es salaam jana mara baada ya kushinda kesi iliyokuwa ikimkabili kuhusiana na ushindi wake kwenye Uchanguzi mkuu wa mwaka 2010.

Mnyika akipongezwa na baadhi ya Jamaa waliofika mahakamani hapo.

Wanachama wa CHADEMA pamoja na washabiki mbalimbali wa Mbunge wa Jimbo la Ubungo  Mh Mnyika wakishangilia Ushindi wa Kesi ya Mbunge wao.

Askari polisi walikuwepo pia kuhakikisha ulinzi wa kutosha katika njia walizopita wapenzi wa CHADEMA kusherehekea ushindi wa Mbunge wa Ubungo.

Mh Mnyika alipokuwa akiwasili mahakamani jana asubuhi.

 Mnyika akisindikizwa kuingia mahakamani jana asubuhi,kushoto ni Diwani wa Sinza, Bw.Renatus Pamba.

 Akisalimiana na Mwenyekiti wa CHADEMA,Mh Freeman Mbowe ndani ya mahakama jana.


PEOPLEEEEEEES!!!!!!!!!

Kutoka Page ya Twitter ya Mnyika:


Ushindi huu ni wetu sote kwani ktk kura elfu60+ ifahamike yangu ni moja tu!Hivyo ushindi huu ni faraja kwa wote walioguswa na ushindi 2010.

1 comment:

Anonymous said...

pongezi nyingi na Mungu akulinde