Sunday, September 2, 2012

Shughuli za kimaendeleo na ujenzi wa chama jimboni Ubungo


Kwa mwezi huu wa Septemba, katika siku za katikati ya wiki nitaendelea na kazi za kuwawakilisha wananchi kwa lengo la kuisimamia  serikali jimboni na kitaifa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kwa siku za mapumziko ya mwisho wa wiki, nitakuwa nafanya matukio na mikutano ya kichama jimboni kwa malengo;
Mosi, kutekeleza programu ya demokrasia na ujenzi wa chama ngazi ya chini katika kata na mitaa mbalimbali.
Pili, kuhamasisha viongozi na wanachama kufuatilia kazi za maendeleo jimboni na kujiandaa kutoa maoni ya mabadiliko ya Katiba Mpya.

Jana Septemba 1, 2012 nilianza kata ya Msigani-Makondeni, Mbezi Hii, Malambamawili, Msingwa, Bwaloni na Masaki ambapo nilizindua misingi, matawi,ofisi na nimepokea wanachama. Aidha nimesomewa risala za masuala ya kufuatilia, nimeulizwa maswali na nimehutubia kama njia moja wapo ya kujibu baadhi ya hoja zenye kuhitaji majibu na ufafanuzi.

Leo Septemba 2, 2012 nitakuwa kata ya Mbezi-Luis; Kilimahewa, Msumi, Msakuzi, Makabe na Mshikamano.

Njoo ushiriki, tulijenge jimbo letu. Kwa pamoja tunaweza.
Maslahi ya Umma Kwanza.

John Mnyika (MB)
Jimboni Ubungo
02 Septemba, 2012

No comments: