Thursday, January 3, 2013

Ufafanuzi wa Waziri Muhongo:ukweli umefichwa, upotoshaji unaendelea!


Nimesoma taarifa ya serikali iliyotolewa na Waziri Prof. Muhongo kufafanua kuhusu miradi ya utafutaji na uvunaji wa gesi asili nchini. Hatimaye serikali imeanza kutoa ufafanuzi suala ambalo ilikwepa kulifanya bungeni hata baada ya kuhoji 2011 na 2012. Hata hivyo ufafanuzi huo haujitoshelezi kwa kuwa kuna ukweli umeendelea kufichwa na upotoshaji umejirudia kama ambavyo nitafafanua katika kauli yangu nitakayotoa siku chache zijazo kwa kuwa leo niko katikati ya kushughulikia usiri na udhaifu katika mikataba na miradi ya Maji jijini Dar es Salaam.

Maslahi ya Umma Kwanza

John Mnyika (MB)
Waziri Kivuli, Nishati na Madini
03 Januari 2013

No comments: