Thursday, February 20, 2014

Kwanini ni muhimu tushirikishe wananchi katika kutunga kanuni za Bunge Maalum

Kwenye kikao cha juzi cha Bunge Maalum nilipendekeza umuhimu wa suala la ushirikishwaji wa wananchi na wadau mbalimbali katika kutengeneza kanuni (Soma hapa: http://goo.gl/b0nQVA) . Wapo wenye mtazamo kwamba kanuni kwa kuwa ni za Bunge Maalum, kuandaa na kupitisha rasimu hiyo ni suala la wajumbe wenyewe pekee; hakuna ulazima wa wadau wala umma kushirikishwa.

Hata hivyo, kwa uzito na unyeti wa kanuni zenyewe na kwa kuzingatia kwamba mjumbe anapaswa kuzingatia maoni ya aliyemtuma ni muhimu umma ujue na kushiriki.

Pia, izingatiwe kwamba Bunge Maalum linapoendelea upo wakati wadau na wananchi wanataka kufuatilia kuhakikisha maoni na maslahi yao yanazingatiwa na wajumbe wao.

Hivyo, ni muhimu kushirikishwa kupata kuwezesha kanuni kuruhusu fursa hiyo. Ni wajulishe tu kwamba rasiu ya Katiba kuchakachuliwa badala ya kuboreshwa. Nitafanya uchambuzi wa vifungu hivyo vibovu na hatimaye nitawasilisha mapendekezo ya maboresho kwa Bunge Maalum.

No comments: