Tuesday, July 18, 2017

Matengenezo ya haraka ya miundo mbinu-Kata ya Saranga

Jana Julai 17 Nilitembelea Kata ya Saranga na kujionea hali duni ya miundombinu ya barabara ambazo zimeharibika vibaya sana.

Kwa hatua ya awali nimekwishafanya mawasiliano na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo na Mkurugenzi wa Dawasco ili nao watembelee na kutuma watendaji kufanya matengenezo kwa haraka.

Nimetoa mwito, maeneo yote mabovu yawekwe kifusi lakini kwa hatua ya kudumu yawekwe slabu za zege kama ilivyofanyika kwenye baadhi ya maeneo kwenye barabara hiyo.

Muhimu: 
Ziara ktk kata zingine tano ndani ya Jimbo letu la Kibamba zinakuja!

John John Mnyika,
Mbunge wa Kibamba,
Julai 18, 2017

No comments: